Tangaza Hapa Email: sales@nifahamishe.com
   
 
Member's Login
Username
Password
Not a member? Sign Up
            Sign Out

 
 
Banana Zoro Aahidi Kuonyesha Makali Yake Mwaka Huu


MWANAMUZIKI na mmiliki wa bendi ya B-Band, Banana Zahir Ally Zorro
Tuesday, January 12, 2010 10:17 PM
MWANAMUZIKI na mmiliki wa bendi ya B-Band, Banana Zahir Ally Zorro ametamba kuwa wanamuziki wa bendi yake akiwemo baba yake mzee Zorro wamejipanga vyema mwaka huu kuhakikisha wanatamba katika medani ya muziki nchini.
Akizungumza na Nifahamishe.com, Banana alisema kuwa mwaka 2009 bendi yake imefanya kazi kubwa na imeweza kuzikonga vilivyo nyoyo za wapenzi wa muziki waliohudhuria katika maonyesho yao.

Banana alisema pamoja na kazi hiyo, lakini mwaka 2010 wanataka kuhakikisha kuwa wanafanya kazi ambayo itawavutia wadau wote wa muziki.

"Unajua sisi lengo letu ni kuwa juu kila wakati. Kwa kuwa mwaka 2009 tumeweza kufanya vyema, hatutaki kuridhika na mafanikio hayo. Tunataka kupiga hatua zaidi na kuwa bendi tishio nchini," alisema Banana.

Mwanamuziki huyo alisema kuwa anaamini hilo litatimia kwani wanamuziki wake akiwemo baba yake Mzee Zahir Ally Zorro ni watu wa kujituma na wenye kiu ya mafanikio.

"Ndani ya B- Band hakuna bosi. Kila mmoja ana kiu ya kuona tunapiga hatua zaidi, ndiyo maana hata ukija kwenye maonyesho yetu unaona namna baba yangu anavyojituma na kuwa sawa na vijana wengine" alisema Banana.

Banana alisema baada ya kutamba na vibao kama Nzela katika mwaka wa 2009, mwaka huu wanatarajia kutoa vibao vingi vipya na kujigamba kuwa anaamini vibao hivyo vitafanya vyema.

 
Na Kalimanzila, Dar    
Mtumie Rafiki Yako
  Comments    Add your Comment

Mtoa Maoni: Ubuguvu    Wednesday, January 13, 2010 00:12:53   
 
Hawa nao sijui ndiyo wasanii kweli au ndiyo wapo ktk kujiali tu jamani sio lazima wote muimbe nani atakua mshabiki BHAI wewe nani promota, mc, projuza au msanii? MOMS016 msanii bongo! Kalimanzila nama umebadilika sijui ndiyo mwaka mpya naona leo habari inasomeka au hii appetizer tu habari kamili inakuja!
 
 
Mtoa Maoni: moms016    Wednesday, January 13, 2010 03:14:05   
 
Mm namkubali Babana, na namuombea mafanikio mema kwa kila hatua yake sio, anajiheshimu kwa kadiri nimjuavyo, kweli nampongeza na anastahiki pongezi.
Ila hawa wanaojiita kurusha roho waache mara moja mabo ya kijinga ya kuiharibu tarabu yetu asilia.
KIPARA c mshabiki wa mambo haya.
Declakers ana kikundi chake tujiandae washabiki!
MINA/DILLY waigizaji wa ngonjera na utenzi mashuleni.. UBUGUVU unajua kucheza chindimba?

 
 
Mtoa Maoni: KING    Wednesday, January 13, 2010 18:04:32   
 
Ha ha ha ha...........MOMS016 kumbe rusha roho yakukera?
Nadhani hawa vijana wa Bongo fleva nao wanachonga sana, kila mwaka wanajipanga? Ln tutaja wasikia anga za kina Salif Keita, Anjelique Kidgo, 2face Idibia, P-Square na Fally Ipupa? Wapunguze maneno, ni muda wa vitendo zaidi kwani muda huwa hausubiri huu. Anyway, KILA LA HERI!

 
 
Mtoa Maoni: Dilly    Friday, January 15, 2010 09:00:53   
 
Unajuaje Moms016. Kweli mi muimbaji wa ngonjera shuleni. Banana yasiwe majigambo tu, fanya kweli basi mtu wangu si unajua tena
 
 
Mtoa Maoni: MINA    Friday, January 15, 2010 10:14:12   
 
MMMh me pia banana ananibamba sana tu but wapo wale wanaotaka kuonekana kwenye video tu rabda momso16, king na ubuguvu na nyinyie muanzishe nifahamishe band me takuwa mc wenu, ubuguvu we utakuwa prodyuza
 
 
       Jumla kuna maoni (6), Soma maoni yote
Unakaribishwa kuchangia maoni yako
Jina Lako    *
Maoni Yako *
 
*** Unaruhusiwa kutuma maoni yako yoyote yale. Tafadhali tumia lugha nzuri, maoni yenye kukashifu watu na yasiyofaa kwa jamii hayataruhusiwa. ***

*** Maoni yanayotolewa hapa ni mawazo binafsi ya Mtoa Maoni
Nifahamishe.com Haihusiki na maoni yatakayotolewa ***
Habari zaidi za burudani
> VIDEO - Si Uchawi ni Mazoezi tu..
> 'Wanamuziki wa Bongo Flava Tungeni Nyimbo zenye Ujumbe'
> 'Miss Kibonge' Apatikana Italia
> Lundega: Miss Tanzania mwaka huu balaa
> Fella Ageukia Qaswida
> Mwisho Arudi kwa Kishindo Big Brother
> Mrembo wa Temeke Apatikana
> Ukimwi na Ushoga Ndani ya Radio Clouds ?
> VIDEO - Chris Brown Adaiwa Kujiliza Jukwaani
> VIDEO - Mtoto Aliyezua Gumzo Kwenye YouTube
> Chris Brown Anyimwa Viza ya Uingereza
> 50 Cent Choka Mbaya, Ukimuona Huwezi Kumtambua
> Burudani Time - Nyama ya Bata
> Mwarabu Kuiwakilisha Marekani Mashindano ya Urembo ya Dunia
> Mrembo Mpya wa IFM Apatikana
> Burudani Time - Angalia Mkuki Usikuchome
> Saleh Kupaza: ‘mchawi’ Aliyepewa Mwana kulea Twanga Pepeta
> 'Nipigie' ya AT Kuingia Sokoni
> Ali Choki na Kupaza Kukumbushia Enzi Zao
> TID na Ali Kiba Nani Mkali Kujulikana Jumapili
> Huku Mvua Ikinyesha, Mzee Yusuf Alamba Alamba Aaaamm...
> VIDEO - 'Tozi wa Mbagala' Kuingia Sokoni Mwezi Ujao
> Nyota wa Bongo Star Search Ajiunga na Mjomba Band
> Kapuya Aweka Uwaziri Pembeni na Kuanza Kupekecha
> Rihanna Amwaga Radhi Kwenye Bethidei Yake

...Habari Zaidi

 

Advertisements
Namabengo Computer Repairing Services Call: 0762-486583 0r 0712-409641
Habari Zilizosomwa Sana
1 'Yesu Alikuwa ni Muathirika w...
Photo Gallery
Photo Album

 Ukisikia Wazazi bomu
Random Photo

 Ashakum
Habari Mpya Mpya
> 'Yesu Alikuwa ni Muathirika wa Ukimwi'
> PICHA - Mapenzi Yanaua..
> Askofu Awaponda Wanaomtukana Kikwete
> Siri ya Kimada Yafichuka
> Ajinyonga Baada ya Kunyimwa Mkopo
> VIDEO - Mwanaume Anayemchezea Simba Sharubu
> Kampeni zachachamaa, wapinzani nao watoa ahadi
> JK aendelea kutoa ahadi
> Pingamizi la Chadema baada ya siku 5
> Urefu Wasababisha Aache Shule ya Msingi