|
|
|
Bendi ya Sikinde Kufungua Matawi Kila Mkoa |

Msemaji wa Sikinde Jimmy Chika, akiwa kazini |
Tuesday, January 12, 2010 10:12 PM
BENDI ya muziki wa dansi ya Orchestra Mlimani Park inatarajia kufungua matawi yake kila mkoa nchini na baadae itakuwa ikiyatembelea matawi hayo kwa ziara za kimuziki. |
Afisa habari wa bendi hiyo Jimmy Chika alisema kwamba maamuzi hayo yamefikiwa na kamati ya utendaji ya bendi hiyo iliyoketi Jumamosi kwa ajili ya kujadili maendeleo ya bendi hiyo kwa mwaka 2010 pamoja na mikakati mipya.
Katika mkakati huo bendi hiyo imo katika mchakato wa kuwasiliana na wapenzi wake wa mikoani ambao pamoja na mambo mengine pia watapatiwa kadi za uanachama na kisha kuelekezwa jinsi ya kuchagua viongozi.
Katibu wa bendi hiyo Hamisi Milambo katika kikao hicho alisema kwamba katika ziara ya bendi hiyo kwenye mikoa ya Mwanza na kisiwani Zanzibar washabiki wao walionyesha ari ya kuunga mkono mpango huo.
Kutokana na mafanikio hayo ya awali Chika aliongeza kuwa baada ya kukamilisha zoezi la kufungua matawi bendi hiyo itaanza ziara ya kutembelea mkoa moja hadi mwingine kwa ajili ya kufungua matawi na pia kufanya maonyesho.
Bendi hiyo hivi sasa inatamba na albam yake ya "Supu umeitia nazi" ambayo ni matunda ya mwimbaji chipukizi Karama Regesu aliyejiunga na bendi hiyo akitokea Msondo ngoma. |
|
|
Na Kalimanzila, Dar
|
|
|
|
|
|
|
|
Mtoa Maoni:
moms016
Wednesday, January 13, 2010 03:43:09
|
|
Mtoa Maoni:
KING
Wednesday, January 13, 2010 18:13:09
|
|
Mtoa Maoni:
mina
Friday, January 15, 2010 10:15:36
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Habari zaidi za burudani |
...Habari Zaidi
|
|
Advertisements

|
|
Habari Zilizosomwa Sana |
|
|
|
|
| Photo Gallery |
 |
|
|
 |
|
|
|
|
|
|
|