|
|
|
Kwanini Watu Wengine Hata Wale Vipi Hawanenepi? Jibu la Kisayansi |

|
Monday, January 04, 2010 2:22 PM
Wakati baadhi ya watu hata wakila kidogo tu vyakula vyenye mafuta huanza kunenepa, kuna wengine hata wale vizuri kiasi gani au wale vyakula vya mafuta kiasi gani huwa hawanenepi hata kidogo, wanasayansi wamepata jibu la suala hilo. |
Wanasayansi wamepata jibu la swali “kwanini watu wengine hata wale vipi hawanenepi?” Jibu ni kwamba kama umezaliwa mwili wako ukiwa hauna vimeng’enyo vya mafuta basi wewe hata ule kiasi gani cha vyakula vyenye mafuta mengi kama vile chips, burger na vinginevyo huwezi kunenepa.
Wanasayansi katika chuo kikuu cha California,San Francisco nchini Marekani wamekigindua kimeng’enyo kinachoitwa MGAT2 ambacho ndicho kinachosimamisha jinsi vyakula tunavyokula vinavyonyonywa mwilini.
Kimeng;enyo cha MGAT2 huamua kama mafuta katika vyakula tunavyokula yaingizwe mwilini au yaondolewe mwilini kwa kugeuzwa kuwa eneji.
Kwa maana hiyo kama mwili wako hauna au kiasi kidogo sana cha kimeng’enyo cha MGAT2 basi unaweza ukala chakula chochote unachotaka bila kuhofia kunenepa kwani mafuta yote hayatakuwa yakihafadhiwa mwilini badala yake yatageuzwa eneji.
Katika majiribio waliyofanyiwa panya, wanasayansi waliwachukua panya wa kawaida na panya wa maabara ambao walikuwa hawana MGAT2, walipowalisha milo isiyo na mafuta mengi, panya wote walifanana ukuaji wao.
Lakini walipowalisha vyakula vya Kimarekani vyenye mafuta asilimia 60, panya wa maabara walikuwa na uzito asilimia 40 pungufu ya panya wa kawaida. Pia panya wa maabara miili yao ilionekana kuwa na mafuta asilimia 50 pungufu ya panya wa kawaida.
Panya waliokosa MGAT2 mbali ya kunusurika na tatizo la unene pia waliepukana na maradhi yanayotokana na unene kama vile maini kujaa mafuta.
Wanasayansi wanaendelea na utafiti zaidi ili kugundua dawa za kupunguza MGAT2 ili kuwafanya watu waweze kula vyakula wanavyopenda kwa kiasi chochote kile bila kuhofia kunenepa. |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Mtoa Maoni:
martin
Monday, January 04, 2010 16:39:34
|
|
Mtoa Maoni:
KING
Monday, January 04, 2010 17:12:34
|
|
Mtoa Maoni:
Dilly
Monday, January 04, 2010 18:27:20
|
|
Mtoa Maoni:
Sauali
Monday, January 04, 2010 21:09:06
|
|
Mtoa Maoni:
moms016
Wednesday, January 06, 2010 19:12:53
|
|
|
|
|
|
Jumla kuna maoni (6), Soma maoni yote |
|
|
|
|
|
|
|
More life style news and articles |
...Habari Zaidi
|
|
Advertisements

|
|
Habari Zilizosomwa Sana |
|
|
|
|
| Photo Gallery |
 |
|
|
 |
|
|
|
|
|
|
|