Tangaza Hapa Email: sales@nifahamishe.com
   
 
Member's Login
Username
Password
Not a member? Sign Up
            Sign Out

 
 
VIDEO - Mtoto wa Miaka 7 Mwenye Albamu Tatu za Muziki


Mtoto Cleopatra Stratan mwenye albamu tatu za muziki
Saturday, December 26, 2009 5:17 AM
Pamoja na kuwa na umri mdogo wa miaka saba, mtoto Cleopatra Satrana raia wa Moldova anayeishi nchini Romania ameishatoa albamu tatu za muziki, ndiye msanii mdogo kuliko wote kulipwa pesa nyingi na ndiye msanii mdogo kuliko wote duniani kushinda tuzo 3 za muziki za MTV.
Mtoto Cleopatra Stratan alizaliwa nchini Moldova mwezi oktoba mwaka 2002 na ndiye anayeshikilia rekodi ya dunia ya kuwa msanii mdogo kuliko wote kupata mafanikio makubwa kwenye biashara ya muziki.

Akiwa na umri wa miaka mitatu, Cleopatra alitoa albamu yake ya kwanza iliyokwenda kwa jina la "La vârsta de trei ani" ambayo aliiuza kwa dola laki tatu ( Takribani Tsh. Milioni 390).

Cleopatra anashikilia rekodi ya kuwa msanii mwenye umri mdogo kufanya shoo ya masaa mawili mbele ya hadhara kubwa ya watu na ndiye msanii mdogo kuliko wote anayelipwa pesa nyingi.

Cleopatra pia anashikilia rekodi ya kuwa msanii mdogo kuliko wote kushinda tuzo tatu za muziki za MTV.

Cleopatra pia ana rekodi nyingine ya kuwa msanii mdogo kuliko wote nyimbo yake kushika namba moja katika chati za muziki duniani. Wimbo wake "Ghita" ulishika namba moja kwenye chati za muziki za Romania na Japan.

Kipaji cha Cleopatra kinatokana na baba yake Pavel Stratan, ambaye ni mwalimu wa muziki.

Wakati Cleopatra baba yake alipokuwa na umri wa miaka mitatu, Baba yake alikuwa akirekodi nyimbo studio wakati Cleopatra akizunguka zunguka ndani ya studio.

Ghafla Cleopatra alichukua maiki na kuanza kuimba nyimbo ya baba yake sambamba naye.

Kila mtu aliyekuwa studio alishangazwa na kipaji cha Cleopatra na huo ndio ukawa mwanzo wa Cleopatra kuingia kwenye biashara ya muziki.

Cleopatra amekuwa akitamba zaidi kwenye nchi za ulaya mashariki akiwa na washabiki wengi sana nchini Romania.

Nyimbo zake zimekuwa zikitafsiriwa katika lugha za kiingereza na kihispania ili ziwafikie watu wa mataifa mbali mbali.

Albamu yake ya pili aliitoa akiwa na umri wa miaka miwili na ilikwenda kwa jina la "La Varsta De 5 Ani" huku nyimbo iliyohiti zaidi ikiwa ni "Zunea Zunea".

Albamu yake ya tatu imetambulishwa nchini Romania wiki hii katika shoo ya nguvu iliyohudhuriwa na mamia ya watu.

Cleopatra amekuwa akitembelea nchi mbali mbali akifanya shoo zake za muziki. Baba yake mbali ya kuwa mpiga gita katika shoo za mwanae pia ndiye meneja wa mtoto huyo mwenye kipaji cha muziki.

Si vibaya kama utaangalia video chini kuona mojawapo ya kazi za msanii huyu mtoto ziliyomfanya atambulike duniani.


VIDEO - Mtoto wa Miaka 7 Mwenye Albamu Tatu za Muziki





 
    
Mtumie Rafiki Yako
  Comments    Add your Comment

Mtoa Maoni: Ubuguvu    Saturday, December 26, 2009 06:16:33   
 
Mtoto wa miaka 7 tajiri kama hivi wakati mimi na MOMS016 hatujui tutakula nini masiki Bhai kuna watu wanazaliwa na bahati zao na wanaishi ktk nchi zinazolinda haki za wanamuzi TZ afande sele analia watu wanavyo iba kazi zake angetajirika yeye wangefaidika wengine na yeye angenelea kua masikini nakumbuka TZ tulikua na muibaji mtoto sijui kafia wapi alikua anajiita melody wenzetu Burundi wanayo wakwao anaitwa dogo A sio tajiri kama huyu wa mika 7 lkn anafadhali sio kama wa kwetu kimaisha aliimba nyimbo za kuanganisha warundi baada ya vita rais kampatia makazi usafiri ulinzi KING mungalie dogo A ktk U2B Kipara mchumba huyu jiandae uoe mzungu na wewe
 
 
Mtoa Maoni: KIPARA     Saturday, December 26, 2009 12:42:49   
 
DAAAAH MDAU UBUGUVU ....... KAMA INGELIWEZEKANA HUYU MTOTO ANGELIKUJA KWETU KUNICHUMBIA MIMI SITOMKATAA KABLA KINA @BHAI NA @MOMS016 HAWAJAANZA KUPIGA MISELE KWAO MSICHANA
 
 
Mtoa Maoni: emma    Saturday, December 26, 2009 13:59:07   
 
kinachonishangaza mimi mnatuambia tuangalie video yake hapo chini kitu ambacho si kweli...nyie nifahamishe kuna tatizo gani la kiufundi mbona mnatunyima raha.....
 
 
Mtoa Maoni: Nyoshi    Saturday, December 26, 2009 14:35:07   
 
Mdau Emma upo wapi wewe?
Mbona sisi video tunaiona
Ipeleke kwa fundi kompyuta yako

 
 
Mtoa Maoni: moms016    Sunday, December 27, 2009 17:20:33   
 
1_UBUGUVU wee acha tu! ndio maana nimechelewe kutoa comment ktk habari hii muda wote nilikuwa nikilia kumlilia marehemu R. Marijani, Hivyo nani ktk Afrika hii aliyemuingia kimuziki? Lkn angalia kifo chake! hakustahiki kufa kifo cha kimaskini (ingawa naamini kafariki masikini wa mali lkn tajiri wa moyo, katuachilia hazina na upendo ambao hata hao v`zi wa awamu za kwanza mpk za mwisho hawatotuachilia)Mungu ampokee R.Marijani na wote waliotangulia kwake!
KIPARA itikia "Emiina wee" basi tu!

 
 
       Jumla kuna maoni (6), Soma maoni yote
Unakaribishwa kuchangia maoni yako
Jina Lako    *
Maoni Yako *
 
*** Unaruhusiwa kutuma maoni yako yoyote yale. Tafadhali tumia lugha nzuri, maoni yenye kukashifu watu na yasiyofaa kwa jamii hayataruhusiwa. ***

*** Maoni yanayotolewa hapa ni mawazo binafsi ya Mtoa Maoni
Nifahamishe.com Haihusiki na maoni yatakayotolewa ***
More life style news and articles
> Kelele za Kimahaba Zamponza
> Urefu Wasababisha Aache Shule ya Msingi
> VIDEO - Nywele Zilizokatiwa Bima ya Dola Milioni 1
> Kweli Mapenzi Hayana Umri...
> Mtoto Mnene Kuliko Wote Duniani
> Maisha Yake Yapo Hatarini Iwapo Atalala
> Utamu na Faida za Tende
> Madada Wanne Wazaa Watoto Wanne Ndani ya Siku Nne
> Babu Aota Mmea wa Njegere Kwenye Mapafu
> Akataa Tsh. Milioni 500 Ili Asiolewe
> Auza Bikira Yake Kwa Tsh. Milioni 500
> 'Mwanaume Mjamzito' Kujifungua Mtoto wa Tatu
> Operesheni za Kurudisha Bikira Zawa Dili Uingereza
> Matiti Yapigwa Pasi Ili Kuzuia Watoto Wasibakwe
> Inakuwaje Wanigeria Wakazaa Mtoto Mzungu?
> VIDEO - Apewa Mkong'oto na Kuozeshwa Mke Kinguvu
> Mrembo Mwenye Matiti Makubwa Kuliko Wote Duniani Apigania Maisha Yake
> Mjadala wa Yai na Kuku Kipi Kilianza Wapata Jibu la Kisayansi
> Nyota wa Filamu za Ngono Anapokuwa Mwalimu wa Sekondari..
> Keki ya Bethidei Kutimiza Miaka 130
> VIDEO - Mtoto Azaliwa na Sura Yenye Kinyago China
> Ili Asifariki Analazimika Kula Kila Baada ya Dakika 15
> Afariki Baada ya Kupewa Taarifa ya Kifo Chake
> Watu Wafupi Wako Kwenye Hatari ya Kufa Kwa Magonjwa ya Moyo
> Hatimaye Sio Mungu Tena..

...Habari Zaidi

 

Advertisements
Tangaza Hapa Email: sales@nifahamishe.com
Habari Zilizosomwa Sana
1 Kanisa Lasisitiza Kuchoma Mot...
2 VIDEO - Simba Alipomgeuza Asu...
3 Kelele za Kimahaba Zamponza
4 Mzungu wa Mtibwa Afukuzwa Nch...
5 Kesi ya Rama yahamishiwa Maha...
6 Wanawake tumieni fursra hii
7 Walimu 14 mbaroni kwa wizi wa...
8 Hatimaye Kanisa Laahirisha Ku...
9 Viagra Ya Saudi Arabia Yazua ...
10 VIDEO ya Salamu za EID MUBARA...
Photo Gallery
Photo Album

 Ukisikia Wazazi bomu
Random Photo

 Duh pole sana
Habari Mpya Mpya
> VIDEO ya Salamu za EID MUBARAK Toka Nifahamishe.Com
> Hatimaye Kanisa Laahirisha Kuchoma Moto Quran
> Viagra Ya Saudi Arabia Yazua Mzozo
> Mzungu wa Mtibwa Afukuzwa Nchini Kwa Lugha Chafu
> Kesi ya Rama yahamishiwa Mahakama Kuu
> Wanawake tumieni fursra hii
> Walimu 14 mbaroni kwa wizi wa mitihani, Songea, Mwanza
> Kanisa Lasisitiza Kuchoma Moto Quran Jumamosi
> Kelele za Kimahaba Zamponza
> VIDEO - Simba Alipomgeuza Asusa Mkufunzi Wake