|
|
|
Beyonce na Jay-Z Wabadilisha Majina Yao |

Beyonce Knowles-Carter |
Saturday, December 26, 2009 3:24 AM
Wanamuziki maarufu wa Marekani, Beyonce na Jay-Z ambao wanaendeleza ndoa yao yenye furaha waliyofunga mwaka jana, wameamua kubadilisha majina yao kwa kuyaunganisha majina ya wazazi wao. |
Msanii maarufu wa muziki wa Hip Hop, milionea Jay-Z ameafikiana na mkewe Beyonce kubadili majina yao ya pili.
Wanandoa hao ambao wote ni moto wa kuotea mbali katika anga ya muziki duniani, wameamua kutumia jina moja lililopatikana baada ya kuunganisha majina ya wazazi wao.
Kuanzia sasa Jay-Z ambaye jina lake halisi ni Shawn Carter atajulikana kama Shawn Knowles-Carter wakati Beyonce atajulikana kama Beyonce Knowles-Carter.
Hatua ya wanandoa hao kuunganisha majina yao ya pili inatokana na maombi ya familia ya Beyonce ambayo haina mtoto wa kiume wa kuendeleza ukoo kutaka kuliendeleza jina la Knowles kupitia Beyonce.
Hata hivyo mbele ya wapenzi wa muziki Beyonce na Jay-Z wataendelea kutumia majina yao ya kisanii. |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Mtoa Maoni:
moms016
Saturday, December 26, 2009 04:01:22
|
|
Mtoa Maoni:
KIPARA
Saturday, December 26, 2009 12:20:28
|
|
Mtoa Maoni:
sep
Sunday, December 27, 2009 20:57:22
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Habari zaidi za burudani |
...Habari Zaidi
|
|
Advertisements

|
|
Habari Zilizosomwa Sana |
|
|
|
|
| Photo Gallery |
 |
|
|
 |
|
|
|
|
|
|
|