Tangaza Hapa Email: sales@nifahamishe.com
   
 
Member's Login
Username
Password
Not a member? Sign Up
            Sign Out

 
 
Mtoto wa Miaka 12 Amzalisha Mama Yake


Mtoto Courtney akiwa na dada yake mpya Pashia
Monday, December 21, 2009 7:37 PM
Mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka 12 amepongezwa kwa ujasiri wake aliouonyesha kwa kugeuka mkunga na kumzalisha mama yake mjamzito mtoto wa kike.
Mama mmoja wa nchini Uingereza anamshukuru sana mtoto wake wa kiume kwa ushujaa wake wa kutoogopa na kumsaidia katika kujifungua mtoto wa kike nyumbani kwake.

Mtoto huyo, Courtney Senior, mwenye umri wa miaka 12, aligeuka mkunga baada ya mama yake Amanda Creak mwenye umri wa miaka 30 alipozidiwa na uchungu na kuingia leba nyumbani kwake.

Courtney alimuongoza mama yake bafuni kabla ya kuita ambulansi.

Lakini kabla ya ambulansi haijafika, mama yake alianza kujifungua na kumfanya Courtney ajitose kumzalisha mama yake.

Courtney alimuongoza mama yake katika hatua zake zote za kumzaa mtoto wake wa kike na alipomaliza alichukua taulo na kumzungushia dada yake mpya na kumkabidhi mama yake.

"Nilishtuka sana lakini sikuogopa, nilijua kila kitu ninachotakiwa kufanya kwakuwa nilishawahi kuona programu ya uzazi kwenye TV, nilikopi kila kitu nilichokiona kwenye programu hiyo", alisema mtoto Courtney.

Amanda ambaye ni mama wa watoto wanne alikuwa akitarajia kujifungua mtoto wa kike aliyempa jina la Pashia siku ya krismasi.

Lakini bila kutarajia aliingia leba siku ya jumanne wiki iliyopita baada ya kuzidiwa na uchungu wa uzazi.

Mtoto Pashia alizaliwa akiwa na afya njema na uzito wa kilo 2.45.

"Courtney ni shujaa wangu, watoto wengi wa umri wake wangeogopa sana lakini yeye wala hakuonyesha kupaniki", alisema Amanda.

"Atakuwa na uhusiano mkubwa zaidi na dada yake kwakuwa yeye ndiye aliyesaidia kuzalishwa kwake", aliendelea kusema mama huyo.

Kwa ushujaa wake aliouonyesha Courtney alizawadia viatu vipya na mama yake.

 
Source: The Sun    
Mtumie Rafiki Yako
  Comments    Add your Comment

Mtoa Maoni: Mwaego    Monday, December 21, 2009 20:12:36   
 
Mhh Jamani mtoto anastahili pongezi lakini kuufungua uchi wa mama yake katika hali hiyo yataka moyo mhh mi hapo simo
 
 
Mtoa Maoni: KIPARA    Monday, December 21, 2009 21:24:05   
 
kesho utasikia kamsaidia baba yake kumvisha kondom
 
 
Mtoa Maoni: Bhai.    Monday, December 21, 2009 21:26:22   
 
Toto Courtney Senior iko sujaa kuba sana, kama ona mama ako kuwa gonjwa ipo marazi tamani mpa dawa pona kabisa kuwa nayo guvu mpya.
Mama iko muhimu sana dani family mara 3 zaidi ya Baba. Manamke jaaliwa na SUBHANA UWA TALLAH namna yake peke ake stahmili miezi 9 sisi iko dani tumbo ya Mama, Toto kwisa kuwa kuba ona nafsi yake iko kama RAMBO, tukana Mama ake, zarau Mama ake, pana sadia Mama ake, pana taka jua Mama ake, piga Mama ake, faza mabo baya bele ona bora kewe yake zaidi na Mama yake.

 
 
Mtoa Maoni: Dogo salim    Monday, December 21, 2009 21:27:35   
 
Ok fine bora kuufungua uchi wa mama kuliko kumuacha ateseke mbaya zaidi hakuna watu sasa utatoka nje ukatafute wakunga wakati kijana upo bora kuokoa maisha maisha ya mama kwani kufunua uchi wa mama kitu gani

kwahiyo kama wewe unge fanyaje labda mpo sehemu ambayo ni mbali na wenzenu kidogo unge wafata ukawaita labda mama yupo mwenge wakunga or wasaidizi wapo gongo la mboto unge mwacha mama ukafate wakunga gongo lamboto sio utakua uchizi huo na sio akili timamu

 
 
Mtoa Maoni: Ubuguvu    Monday, December 21, 2009 22:02:58   
 
Wazungu sifa hapana cha ushujaa wala nini kwanza wanawake wanatofautiana ktk kuzaa kuna wanaopata tabu kutokana na maumbile yao mpa daktari aingize mkono na azibe sehemu ya pili ili aweze kujikamua mtoto atoke na wapo wale wasiopata tabu wanazaa na wanafanya kazi zao kama kawaida kama yule mama wa india aliejifungua ktk choo cha treni na mtoto kutumbukia chooni hata kama angekua na kipofu angezaa tu huyu mtoto alisimama tu wakati mama yake anajifungua kaona hapo alipotoka tu uingera ukijifungua siku ya krismasi zinakuja TV kuahoji wazazi sasa huyu kajifungua kabla ya siku anazusha lolote lile ili andikwe
 
 
       Jumla kuna maoni (10), Soma maoni yote
Unakaribishwa kuchangia maoni yako
Jina Lako    *
Maoni Yako *
 
*** Unaruhusiwa kutuma maoni yako yoyote yale. Tafadhali tumia lugha nzuri, maoni yenye kukashifu watu na yasiyofaa kwa jamii hayataruhusiwa. ***

*** Maoni yanayotolewa hapa ni mawazo binafsi ya Mtoa Maoni
Nifahamishe.com Haihusiki na maoni yatakayotolewa ***
More life style news and articles
> Urefu Wasababisha Aache Shule ya Msingi
> VIDEO - Nywele Zilizokatiwa Bima ya Dola Milioni 1
> Kweli Mapenzi Hayana Umri...
> Mtoto Mnene Kuliko Wote Duniani
> Maisha Yake Yapo Hatarini Iwapo Atalala
> Utamu na Faida za Tende
> Madada Wanne Wazaa Watoto Wanne Ndani ya Siku Nne
> Babu Aota Mmea wa Njegere Kwenye Mapafu
> Akataa Tsh. Milioni 500 Ili Asiolewe
> Auza Bikira Yake Kwa Tsh. Milioni 500
> 'Mwanaume Mjamzito' Kujifungua Mtoto wa Tatu
> Operesheni za Kurudisha Bikira Zawa Dili Uingereza
> Matiti Yapigwa Pasi Ili Kuzuia Watoto Wasibakwe
> Inakuwaje Wanigeria Wakazaa Mtoto Mzungu?
> VIDEO - Apewa Mkong'oto na Kuozeshwa Mke Kinguvu
> Mrembo Mwenye Matiti Makubwa Kuliko Wote Duniani Apigania Maisha Yake
> Mjadala wa Yai na Kuku Kipi Kilianza Wapata Jibu la Kisayansi
> Nyota wa Filamu za Ngono Anapokuwa Mwalimu wa Sekondari..
> Keki ya Bethidei Kutimiza Miaka 130
> VIDEO - Mtoto Azaliwa na Sura Yenye Kinyago China
> Ili Asifariki Analazimika Kula Kila Baada ya Dakika 15
> Afariki Baada ya Kupewa Taarifa ya Kifo Chake
> Watu Wafupi Wako Kwenye Hatari ya Kufa Kwa Magonjwa ya Moyo
> Hatimaye Sio Mungu Tena..
> Baada ya Ajali Mtoto wa Miaka 3 Awa Chapombe na Mvutaji Sigara

...Habari Zaidi

 

Advertisements
Tangaza Hapa Email: sales@nifahamishe.com
Habari Zilizosomwa Sana
1 'Yesu Alikuwa ni Muathirika w...
Photo Gallery
Photo Album

 Ukisikia Wazazi bomu
Random Photo

 Ashakum
Habari Mpya Mpya
> 'Yesu Alikuwa ni Muathirika wa Ukimwi'
> PICHA - Mapenzi Yanaua..
> Askofu Awaponda Wanaomtukana Kikwete
> Siri ya Kimada Yafichuka
> Ajinyonga Baada ya Kunyimwa Mkopo
> VIDEO - Mwanaume Anayemchezea Simba Sharubu
> Kampeni zachachamaa, wapinzani nao watoa ahadi
> JK aendelea kutoa ahadi
> Pingamizi la Chadema baada ya siku 5
> Urefu Wasababisha Aache Shule ya Msingi