Tangaza Hapa Email: sales@nifahamishe.com
   
 
Member's Login
Username
Password
Not a member? Sign Up
            Sign Out

 
 
Mtoto wa Mwaka Mmoja Mwenye Uwezo Mkubwa wa Kuogelea


Mtoto Gibson Walker mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu akiogelea
Wednesday, December 16, 2009 2:32 AM
Mtoto Gibson Walker wa nchini Australia pamoja na kuwa na umri wa mwaka mmoja na nusu anawashangaza watu wengi kwa uwezo wake wa kuogelea kiasi cha kwamba huwashinda hata baadhi ya watu wazima.
Mtoto Gibson Walker ana umri wa miezi 18 tu lakini ana uwezo wa kuogelea na kupiga raundi nne katika bwawa la kuogelea lenye urefu wa mita 25.

Akifanya mazoezi katika kituo cha mazoezi ya kuogelea cha Gulliver Coomera Swim Centre, Gibson huogelea kwa mwendo kobe wa taratibu lakini hufanikiwa kumaliza raundi nne kuzunguka bwawa la kuogelea bila kupumzika.

Baba yake Gibson, Mark alisema kuwa alianza kumfundisha mwanae kuogelea tangia alipokuwa na umri wa miezi sita na ghafla alianza kupenda kuogelea.

"Anajiamini sana anapoogelea kiasi cha kunifanya nisiwe na hofu yoyote", alisema baba wa mtoto huyo.

Mafunzo ya kuogelea aliyopewa akiwa na umri mdogo yalimsaidia mtoto huyo kuokoa maisha yake wakati alipodondoka pembeni ya bwawa la kuogelea na kuangukia kichwa kabla ya kuangukia kwenye bwawa la kogelea.

Gibson badala ya kuanza kulia kama watoto wenzake ambavyo wangefanya, aliogelea hadi kwenye ukingo wa bwawa hilo na kujitoa mwenyewe nje ya bwawa hilo ndipo akaanza kulia.

Mwalimu wake wa kuogelea Terry Gulliver ana rekodi nzuri ya kuwafundisha watoto wenye umri mdogo kuogelea. Aliwahi kumfundisha mtoto wa miaka mitatu kuweza kuogelea mita 1500 bila matatizo yoyote.

"Kuogelea ni mchezo muhimu sana kwa maisha yetu", alisema Gulliver.

"Idadi ya watu wanaofariki kwa kuzama katika maji ingepungua kama watoto wote wangefundishwa kuogelea angalau mita chache", alimalizia kusema mwalimu huyo wa kuogelea.

 
Source: News Agencies    
Mtumie Rafiki Yako
  Comments    Add your Comment

Mtoa Maoni: Ubuguvu    Wednesday, December 16, 2009 09:17:53   
 
Vipaji kama hivi TZ vimejaa lakini vigumu kuvigundua mapema maji ya kunywa watu hawana watakua na maji ya kuchezea! KING umri kama huu tulikua tunaogeshwa ktk beseni vigumu kugundulika vipaji vyetu nampongeza huyu mzazi kumfundisha mwanae vitu vya maana na sio kunfunza mwanao kusukuma magari na mikokote na hapa wazazi wengi tunakosea mara nyingi tunawalazimisha watoto wentu wapende tunachokipenda sisi hata kama kipaji sio chake mara chache sana watoto kua na vipaji sawa na wazazi wao au sehemu anayotoka na hata akiwa nacho cha kulazimisha kama maximo na ukocha MOMS016 hata ukilazimisha uchungaji mwisho utabaka tu
 
 
Mtoa Maoni: KING    Wednesday, December 16, 2009 09:38:47   
 
Ha ha ha UBUGUVU kwa Tz labda wakajifunzie kwenye madimbwi ya barabarani, heri yetu cc tuliozaliwa kando ya mito na majosho ya ng'ombe huko bara mbizi shwaaaari kabisa labda na MOMS016 pamoja na wadau wengine wa visiwani manake huko kuionja pwani lazima, shaka yangu ni BHAI, AMANKWA, KIPARA na DE CLARKES kama waweza koga bila kuvalishwa 'tube'. Anyway, career nzuri hii kanaweza kuwa karithi ka Michael Phelps siku zijazo, inshallah!
 
 
Mtoa Maoni: DeClarkes    Wednesday, December 16, 2009 10:21:35   
 
Sina uhakika kwamba mtoto wa miezi 18 ameshapata akili kiasi cha kutambua baya na zuri. Nadhani mazingira ya kumfanya aoge ni sawa na kumpa mkono simba alambe. Ushauri wa bure, ni vizuri kwa maonyesho kuwapa mazoezi watoto wadogo hivyo lakini yakiwakuta msilie akina KING.
 
 
Mtoa Maoni: mkaliwam    Wednesday, December 16, 2009 10:22:13   
 
kweli kila mtu na kipaji chake,wabongo tunaforciwa kufanya kitu ambacho co kipaji chetu.Mtu analazimishwa kuwa daktari wakati kipaji chake ususi.unathani tutafika?
 
 
Mtoa Maoni: kadudu    Wednesday, December 16, 2009 14:57:04   
 
kweli kabisa jamani watanzania wanalazimisha vipaji kabisa maana mtoto utamjua na kipaji akiwa bado mdogo tu akiwa mkubwa basi utakuwa umeshajua anapenda nini
 
 
       Jumla kuna maoni (10), Soma maoni yote
Unakaribishwa kuchangia maoni yako
Jina Lako    *
Maoni Yako *
 
*** Unaruhusiwa kutuma maoni yako yoyote yale. Tafadhali tumia lugha nzuri, maoni yenye kukashifu watu na yasiyofaa kwa jamii hayataruhusiwa. ***

*** Maoni yanayotolewa hapa ni mawazo binafsi ya Mtoa Maoni
Nifahamishe.com Haihusiki na maoni yatakayotolewa ***
More life style news and articles
> Urefu Wasababisha Aache Shule ya Msingi
> VIDEO - Nywele Zilizokatiwa Bima ya Dola Milioni 1
> Kweli Mapenzi Hayana Umri...
> Mtoto Mnene Kuliko Wote Duniani
> Maisha Yake Yapo Hatarini Iwapo Atalala
> Utamu na Faida za Tende
> Madada Wanne Wazaa Watoto Wanne Ndani ya Siku Nne
> Babu Aota Mmea wa Njegere Kwenye Mapafu
> Akataa Tsh. Milioni 500 Ili Asiolewe
> Auza Bikira Yake Kwa Tsh. Milioni 500
> 'Mwanaume Mjamzito' Kujifungua Mtoto wa Tatu
> Operesheni za Kurudisha Bikira Zawa Dili Uingereza
> Matiti Yapigwa Pasi Ili Kuzuia Watoto Wasibakwe
> Inakuwaje Wanigeria Wakazaa Mtoto Mzungu?
> VIDEO - Apewa Mkong'oto na Kuozeshwa Mke Kinguvu
> Mrembo Mwenye Matiti Makubwa Kuliko Wote Duniani Apigania Maisha Yake
> Mjadala wa Yai na Kuku Kipi Kilianza Wapata Jibu la Kisayansi
> Nyota wa Filamu za Ngono Anapokuwa Mwalimu wa Sekondari..
> Keki ya Bethidei Kutimiza Miaka 130
> VIDEO - Mtoto Azaliwa na Sura Yenye Kinyago China
> Ili Asifariki Analazimika Kula Kila Baada ya Dakika 15
> Afariki Baada ya Kupewa Taarifa ya Kifo Chake
> Watu Wafupi Wako Kwenye Hatari ya Kufa Kwa Magonjwa ya Moyo
> Hatimaye Sio Mungu Tena..
> Baada ya Ajali Mtoto wa Miaka 3 Awa Chapombe na Mvutaji Sigara

...Habari Zaidi

 

Advertisements
Namabengo Computer Repairing Services Call: 0762-486583 0r 0712-409641
Habari Zilizosomwa Sana
1 'Yesu Alikuwa ni Muathirika w...
Photo Gallery
Photo Album

 Ukisikia Wazazi bomu
Random Photo

 Ashakum
Habari Mpya Mpya
> 'Yesu Alikuwa ni Muathirika wa Ukimwi'
> PICHA - Mapenzi Yanaua..
> Askofu Awaponda Wanaomtukana Kikwete
> Siri ya Kimada Yafichuka
> Ajinyonga Baada ya Kunyimwa Mkopo
> VIDEO - Mwanaume Anayemchezea Simba Sharubu
> Kampeni zachachamaa, wapinzani nao watoa ahadi
> JK aendelea kutoa ahadi
> Pingamizi la Chadema baada ya siku 5
> Urefu Wasababisha Aache Shule ya Msingi