Tangaza Hapa Email: sales@nifahamishe.com
   
 
Member's Login
Username
Password
Not a member? Sign Up
            Sign Out

 
 
Mtoto wa Miaka 6 Mwenye Uwezo wa Kuvuta Magari


Mtoto Santhosperumal akionyesha uwezo wake wa kuvivuta vitu vyenye uzito mkubwa
Monday, December 14, 2009 10:03 PM
Pamoja na kuwa na umri wa miaka 6 tu, mtoto huyu wa nchini Malaysia amewashangaza watu wengi kwa uwezo wake wa kulivuta gari lenye uzito wa tani mbili.
Mtoto T. Santhosperumal wa mji wa Klang nchini Malaysia amejipatia umaarufu mkubwa kwa uwezo wake wa kuvivuta vitu vyenye uzito mkubwa ambavyo hata baadhi ya watu wazima wasingeweza hata kuvisogeza achilia mbali kuvivuta kwa mita kadhaa.

Akitumia mkanda uliofungwa kiunoni mwake, mtoto huyo alifanikiwa kulivuta gari lenye uzito wa tani 1.650 mbele ya mamia ya watu waliojazana kushuhudia uwezo wake.

Baba wa mtoto huyo, N. Thiagu, alijivunia uwezo wa mtoto wake na alisema kuwa anaamini siku moja mtoto wake atavunja rekodi ya dunia.

"Santhosperumal, ana uwezo wa kufanya kila kitu anachotaka kufanya au kujifunza, alipokuwa na umri wa miaka minne alianza kuendesha gari hivi sasa anaweza kuendesha hata malori", alisema baba wa mtoto huyo.

Mama wa mtoto huyo naye alijivunia maguvu ya mwanae na kuongeza kuwa mtoto wake anakula chakula sawa na watoto wengine hamna lishe maalumu anayopewa.

Santhosperumal anapenda kuangalia katuni kama watoto wengine isipokuwa katuni anazozipendelea zaidi ni zile zinazoonyesha matumizi ya nguvu katika shughuli mbali mbali.

"Siku moja nitawaonyesha watu uwezo wangu kwa kuivuta ndege", alitamba mtoto huyo.

 
    
Mtumie Rafiki Yako
  Comments    Add your Comment

Mtoa Maoni: moms016    Monday, December 14, 2009 22:35:31   
 
mhh, si kama wtt km hawa hawapo tz, lkn wkt bb uko wp? hajalikani mtt wl bb kwa kuchoka, "maisha bora kwa kila mtz" Labda gari za wahindi!
Hogera kwa wazazi muhimu asiwe mtukutu tu wa kuwapa mkongoto wenziwe!
Halafu hili jina au treni?

 
 
Mtoa Maoni: Ubuguvu    Tuesday, December 15, 2009 01:11:23   
 
MOMS016 labda gari ya mabua mtoto miaka 4 unaendesha gari! hapa nampongeza amenipita mimi nilipokua na miaka 10 nikipata mbele tu mtaani kote watapata habari lakini na hao wanaompa marori wana akili au nawao wanumwa kama huyu mtoto hizi ndiyo sifa za kijinga mtoto ndogo anavuta gari sasa ndiyo iwe nini mtoto usifiwa kipaji cha kumjenga kimwili kiafya na kiakili asiachiwe na hii tabia yake itamuaribu wazazi wafanye haraka kumtibia huyo mtoto kipara wewe ukijaribu kuvuta gari vitu vitatoka chini na juu
 
 
Mtoa Maoni: soud    Tuesday, December 15, 2009 03:35:45   
 
Huyu mtoto anaonekana ana JINI linalo Msaidia
 
 
Mtoa Maoni: DeClarkes    Tuesday, December 15, 2009 10:24:40   
 
Na wasiwasi sana kama ni kipaji ama ni ajira? Kwanza ni mtoto wa miaka sita maana hajui a wala be sidhani kama angekua hata darasa la kwanza hapa Bongo. Ushauri wa bure, kwa wazazi wake wasilewe na mipesa isiyo na dili wampeleke shule asije akapata ngiri bure ama afe ghafla. Moms016 nakufagilia mheshimiwa!
 
 
Mtoa Maoni: SONGA SONGA    Tuesday, December 15, 2009 11:14:00   
 
angekuwa mtoto wangu nisingemruhusu kwani huyu mtoto badae atapata matatizo kama dio mambo ya kishetani!!!!
 
 
       Jumla kuna maoni (12), Soma maoni yote
Unakaribishwa kuchangia maoni yako
Jina Lako    *
Maoni Yako *
 
*** Unaruhusiwa kutuma maoni yako yoyote yale. Tafadhali tumia lugha nzuri, maoni yenye kukashifu watu na yasiyofaa kwa jamii hayataruhusiwa. ***

*** Maoni yanayotolewa hapa ni mawazo binafsi ya Mtoa Maoni
Nifahamishe.com Haihusiki na maoni yatakayotolewa ***
More life style news and articles
> Kelele za Kimahaba Zamponza
> Urefu Wasababisha Aache Shule ya Msingi
> VIDEO - Nywele Zilizokatiwa Bima ya Dola Milioni 1
> Kweli Mapenzi Hayana Umri...
> Mtoto Mnene Kuliko Wote Duniani
> Maisha Yake Yapo Hatarini Iwapo Atalala
> Utamu na Faida za Tende
> Madada Wanne Wazaa Watoto Wanne Ndani ya Siku Nne
> Babu Aota Mmea wa Njegere Kwenye Mapafu
> Akataa Tsh. Milioni 500 Ili Asiolewe
> Auza Bikira Yake Kwa Tsh. Milioni 500
> 'Mwanaume Mjamzito' Kujifungua Mtoto wa Tatu
> Operesheni za Kurudisha Bikira Zawa Dili Uingereza
> Matiti Yapigwa Pasi Ili Kuzuia Watoto Wasibakwe
> Inakuwaje Wanigeria Wakazaa Mtoto Mzungu?
> VIDEO - Apewa Mkong'oto na Kuozeshwa Mke Kinguvu
> Mrembo Mwenye Matiti Makubwa Kuliko Wote Duniani Apigania Maisha Yake
> Mjadala wa Yai na Kuku Kipi Kilianza Wapata Jibu la Kisayansi
> Nyota wa Filamu za Ngono Anapokuwa Mwalimu wa Sekondari..
> Keki ya Bethidei Kutimiza Miaka 130
> VIDEO - Mtoto Azaliwa na Sura Yenye Kinyago China
> Ili Asifariki Analazimika Kula Kila Baada ya Dakika 15
> Afariki Baada ya Kupewa Taarifa ya Kifo Chake
> Watu Wafupi Wako Kwenye Hatari ya Kufa Kwa Magonjwa ya Moyo
> Hatimaye Sio Mungu Tena..

...Habari Zaidi

 

Advertisements
Tangaza Hapa Email: sales@nifahamishe.com
Habari Zilizosomwa Sana
1 Kanisa Lasisitiza Kuchoma Mot...
2 VIDEO - Simba Alipomgeuza Asu...
3 Kelele za Kimahaba Zamponza
4 Mzungu wa Mtibwa Afukuzwa Nch...
5 Kesi ya Rama yahamishiwa Maha...
6 Wanawake tumieni fursra hii
7 Walimu 14 mbaroni kwa wizi wa...
8 Hatimaye Kanisa Laahirisha Ku...
9 Viagra Ya Saudi Arabia Yazua ...
10 VIDEO ya Salamu za EID MUBARA...
Photo Gallery
Photo Album

 Ukisikia Wazazi bomu
Random Photo

 Duh pole sana
Habari Mpya Mpya
> VIDEO ya Salamu za EID MUBARAK Toka Nifahamishe.Com
> Hatimaye Kanisa Laahirisha Kuchoma Moto Quran
> Viagra Ya Saudi Arabia Yazua Mzozo
> Mzungu wa Mtibwa Afukuzwa Nchini Kwa Lugha Chafu
> Kesi ya Rama yahamishiwa Mahakama Kuu
> Wanawake tumieni fursra hii
> Walimu 14 mbaroni kwa wizi wa mitihani, Songea, Mwanza
> Kanisa Lasisitiza Kuchoma Moto Quran Jumamosi
> Kelele za Kimahaba Zamponza
> VIDEO - Simba Alipomgeuza Asusa Mkufunzi Wake