Tangaza Hapa Email: sales@nifahamishe.com
   
 
Member's Login
Username
Password
Not a member? Sign Up
            Sign Out

 
 
Familia Inayoongea na Watu Waliofariki


Kylie na watoto wake wanaodaiwa kuwaona mizimu na kuzungumza na watu waliokufa
Saturday, December 05, 2009 3:02 PM
Familia hii ya nchini Uingereza inadai kuwa na uwezo mkubwa wa kuwaona malaika, mizimu na kuzungumza na watu waliokufa.
Kylie Holmes, mama wa watoto watatu anadai kuwa na uwezo wa kuwaona malaika wakati watoto wake Jade mwenye umri wa miaka 11, Amba mwenye umri wa miaka 9 na Leo mwenye umri wa miaka 5 wanadaiwa kuwa na uwezo wa kuzungumza na kuona vitu ambavyo watu wengine hawavioni wala hawavisikii.

Mtoto Jade yeye ana uwezo wa kukumbuka matukio yaliyopita, Amba ana uwezo wa kuyaona mizimu wakati Leo anadaiwa kuwa na uwezo wa kuongea na watu waliokufa.

"Wamekuwa wakiona na kusikia vitu ambavyo wengine hawavioni wala kuvisikia, Hali hii imekuwa ikitokea katika maisha yao ya kila siku", alisema mama wa watoto hao alipokuwa akiongea na gazeti la The Sun la Uingereza.

Kylie anasema kuwa yeye na watoto wao wamekuwa wakitembelewa na mamia ya watu kila siku wanaotaka kuzungumza na ndugu zao waliokufa na watu wengine wanaotaka kutibiwa matatizo yao.

Mtoto wake mmoja huchora michoro ya ajabu ajabu isiyoeleweka akielezea matukio yaliyopita na yajayo.

Kylie alisema kuwa alianza kuwaona malaika alipokuwa na umri wa miaka 20 baada ya kulazwa hospitali alipomeza dozi kubwa ya dawa kufuatia stress za matatizo katika mahusiano yake ya kimapenzi.

Kylie anasisitiza kuwa alipoamka hospitalini aliona mwanga ulio kwenye umbile la mtu ambao ulimwambia kuwa atapona.

Anasema kuwa alipopona na kurudi nyumbani kwake alishangaa kukuta chumba chake kimepambwa na manyoya meupe ya ndege na malaika aliyemuona hospitali alimtokea tena.

Kylie anadai kuwa tangia siku hiyo amekuwa akiwasiliana na malaika wake ambaye amekuwa akimsaidia kuyatatua matatizo ya watu wanaofika nyumbani kwake.

Hata hivyo mume wa Kylie, Bw. Eic ambaye ni mwanajeshi mstaafu ambaye pia ndiye baba wa watoto hao haamini kuwa mkewe na watoto wake wana uwezo wanaodai kuwa nao.

"Hawafanyi kitendo chochote cha kumdhuru mtu .. lakini mimi siamini hata kidogo wanachokisema", alisema Eric.

 
    
Mtumie Rafiki Yako
  Comments    Add your Comment

Mtoa Maoni: ubuguvu    Saturday, December 05, 2009 17:31:07   
 
Familia hizi mbona bongo zipo tunaziita Familia za waganga wa kienyeji wanauezo wa kuongea na invisible piople na wanaweza kukufanya uwe invisible to everyone mara nyingi hutumia majambazi majuu kinachowasidia media kila kitu kinarushwa hewani bongo wapo wengi familia ya wapiganaji matumla, yahaya ..... anakwambia mpaka kesha utakula nini ukienda Tanga watu wanauezo wakukugeuza paka. KING upo?
 
 
Mtoa Maoni: dayame 2005    Saturday, December 05, 2009 19:42:35   
 
@ ubuguvu.... ha ha ha ha ha ha ha
 
 
Mtoa Maoni: moms016    Saturday, December 05, 2009 19:45:02   
 
wakakojoe wakalale! pumba 2pu!
 
 
Mtoa Maoni: Ntarambe    Saturday, December 05, 2009 21:55:30   
 
Hata wao ni watafutaji kwa nini baba mzazi asiwaamini? wasituingize mjini,wao sio manabii.
 
 
Mtoa Maoni: muyomba    Saturday, December 05, 2009 23:03:42   
 
kabisaaaaaaaaa wamekosakazi sasawanatka kutumiautapeli wasitudanganye hiohaiwezekani hatakidogo
 
 
       Jumla kuna maoni (9), Soma maoni yote
Unakaribishwa kuchangia maoni yako
Jina Lako    *
Maoni Yako *
 
*** Unaruhusiwa kutuma maoni yako yoyote yale. Tafadhali tumia lugha nzuri, maoni yenye kukashifu watu na yasiyofaa kwa jamii hayataruhusiwa. ***

*** Maoni yanayotolewa hapa ni mawazo binafsi ya Mtoa Maoni
Nifahamishe.com Haihusiki na maoni yatakayotolewa ***
More life style news and articles
> Kelele za Kimahaba Zamponza
> Urefu Wasababisha Aache Shule ya Msingi
> VIDEO - Nywele Zilizokatiwa Bima ya Dola Milioni 1
> Kweli Mapenzi Hayana Umri...
> Mtoto Mnene Kuliko Wote Duniani
> Maisha Yake Yapo Hatarini Iwapo Atalala
> Utamu na Faida za Tende
> Madada Wanne Wazaa Watoto Wanne Ndani ya Siku Nne
> Babu Aota Mmea wa Njegere Kwenye Mapafu
> Akataa Tsh. Milioni 500 Ili Asiolewe
> Auza Bikira Yake Kwa Tsh. Milioni 500
> 'Mwanaume Mjamzito' Kujifungua Mtoto wa Tatu
> Operesheni za Kurudisha Bikira Zawa Dili Uingereza
> Matiti Yapigwa Pasi Ili Kuzuia Watoto Wasibakwe
> Inakuwaje Wanigeria Wakazaa Mtoto Mzungu?
> VIDEO - Apewa Mkong'oto na Kuozeshwa Mke Kinguvu
> Mrembo Mwenye Matiti Makubwa Kuliko Wote Duniani Apigania Maisha Yake
> Mjadala wa Yai na Kuku Kipi Kilianza Wapata Jibu la Kisayansi
> Nyota wa Filamu za Ngono Anapokuwa Mwalimu wa Sekondari..
> Keki ya Bethidei Kutimiza Miaka 130
> VIDEO - Mtoto Azaliwa na Sura Yenye Kinyago China
> Ili Asifariki Analazimika Kula Kila Baada ya Dakika 15
> Afariki Baada ya Kupewa Taarifa ya Kifo Chake
> Watu Wafupi Wako Kwenye Hatari ya Kufa Kwa Magonjwa ya Moyo
> Hatimaye Sio Mungu Tena..

...Habari Zaidi

 

Advertisements
Tangaza Hapa Email: sales@nifahamishe.com
Habari Zilizosomwa Sana
1 Kanisa Lasisitiza Kuchoma Mot...
2 VIDEO - Simba Alipomgeuza Asu...
3 Kelele za Kimahaba Zamponza
4 Mzungu wa Mtibwa Afukuzwa Nch...
5 Kesi ya Rama yahamishiwa Maha...
6 Wanawake tumieni fursra hii
7 Walimu 14 mbaroni kwa wizi wa...
8 Hatimaye Kanisa Laahirisha Ku...
9 Viagra Ya Saudi Arabia Yazua ...
10 VIDEO ya Salamu za EID MUBARA...
Photo Gallery
Photo Album

 Ukisikia Wazazi bomu
Random Photo

 Duh pole sana
Habari Mpya Mpya
> VIDEO ya Salamu za EID MUBARAK Toka Nifahamishe.Com
> Hatimaye Kanisa Laahirisha Kuchoma Moto Quran
> Viagra Ya Saudi Arabia Yazua Mzozo
> Mzungu wa Mtibwa Afukuzwa Nchini Kwa Lugha Chafu
> Kesi ya Rama yahamishiwa Mahakama Kuu
> Wanawake tumieni fursra hii
> Walimu 14 mbaroni kwa wizi wa mitihani, Songea, Mwanza
> Kanisa Lasisitiza Kuchoma Moto Quran Jumamosi
> Kelele za Kimahaba Zamponza
> VIDEO - Simba Alipomgeuza Asusa Mkufunzi Wake