|
|
|
Mrisho Mpoto Aanzisha Bendi Yake inayoitwa 'Mjomba' |

Mrisho Mpoto |
Friday, November 27, 2009 11:52 PM
Mwamamuziki nyota wa kugh'ani Mrisho Mpoto ameanzisha bendi yake ijulikanayo kwa jina la Mjomba bendi na kuwaahidi washabiki wake kuwa bendi hiyo itakuwa moto wa kuotea mbali. |
Akizungumza na Nifahamishe katika mahojiano maalumu yaliyofanyika katika hoteli ya Ubungo Plazza alisema nia ya kuanzisha bendi hiyo ni kutaka kukidhi matakwa ya wapenzi wake.
Mjomba bendi inaundwa na wanamuziki kumi ambao wametoka sehemu mbalimbali na kuamua kuunda kundi hilo ambalo kiongozi mkuu ni Mpoto.
Kiongozi mwimbaji Ismail Shabani (kapila) alisema kuwa bendi hiyo imeundwa mwaka huu na bado hawajapata sehemu ya kupigia ila kwa sasa wanafanya mazoezi katika ukumbi uliopo Mbezi Tangi Bovu.
Mpoto aliwataja waimbaji waliopo kwenye bendi hiyo kuwa ni mshiriki wa shindano la kutafuta vipaji (BSS) ambaye alifika katika kumi bora na kutolewa katika nafasi ya sita bora Merry Lucos, Abuu mwana wa Zanzibar na Esmail Kipila.
Wengine ambao wanaunda kundi hilo wakiwa katika nafasi mabalimbali aliwataja kuwa ni pamoja na Nuruce, Bcb, Sija, Mlanda, Mbwana Mponda, Joji Choka, Peter na Choyoha.
Tangu kuanzishwa kwa bendi hiyo kumekuwa na manufaa makubwa kutokana na bendi hiyo kupata mialiko mingi ya kiserikali kwenda kutumbuiza katika shughuli mbalimbali za kiserikali.
Kiongozi huyo wa waimbaji alisema bendi hiyo imekuja kuleta burudani kwa wananchi hasa wale wapenda muziki wa dansi na kutabainisha kuwa bendi hiyo ina kila kitu ikiwemo michezo ya maigizo.
Bendi imeanza vizuri sana tofauti na tulivyofikiria mwanzoni na hii imetokana na baadhi ya watu hasa wanamuziki wakongwe kutueleza kuwa tuanzishe bendi tuwe tunapiga live siyo kukopi, alisema Ismail.
Kwa upande wake alipoulizwa kiongozi huyo kuhusiana na soko la muziki hapa nchini alisema kuwa wao wamejipanga vizuri kibiashara na kutoa burudani kwa ujumla alipoulizwa ni bendi gani ambayo anaipenda alisema hakuna bendi zaidi ya Msondo ngoma.
Mrisho Mpoto amejipatia umarufu mkubwa hapa nchini kutokana na aina ya muziki wake anaoupiga.
Kwa kipindi hiki amekuwa akivuma na wimbo wake ambao umempa umarufu wa "Mjomba nikipata nauli nitarudi".
Mjomba hakupenda kutaja umri wake ila alisema kuwa yeye ni baba wa watoto wawili wote wa kiume ambao aliwataja kuwa wa kwanza anaitwa Manjo na wa pili anaitwa Mrisho. |
|
|
Na Kaimanzila, Dar
|
|
|
|
|
|
|
|
Mtoa Maoni:
DeClarkes
Saturday, November 28, 2009 11:37:55
|
|
Mtoa Maoni:
mtenya kitwana
Wednesday, March 17, 2010 14:46:43
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Habari zaidi za burudani |
...Habari Zaidi
|
|
Advertisements

|
|
Habari Zilizosomwa Sana |
|
|
|
|
| Photo Gallery |
 |
|
|
 |
|
|
|
|
|
|
|