|
|
|
Chokoraa Apigwa Stop Twanga Pepeta |

Khalid Chokoraa |
Friday, November 27, 2009 10:52 AM
RAPA wa bendi ya Twanga International, Khalid Chuma ‘Chokoraa’ amesimamishwa na uongozi wa bendi hiyo kutokana na sababu za kuchochea tabia ya utovu wa nidhamu ndani ya bendi. |
Habari za kusimamishwa kwa msanii huyo zilipatikana Jumatano usiku katika ukumbi wa Club Bilicanas ambapo msanii huyo anakabiliwa na shutuma za kuanzisha kundi la Mapacha Wanne ambako wamekuwa wakifanya kazi bila ya kupata idhini kwa mwajiri wao.
Mkurugenzi Mtendaji wa bendi ya hiyo, Asha Baraka, alisema ndani ya ukumbi wa Club Bilicanas kwamba wamefikia hatua hiyo kwakuwa Chokoraa ndiye kinara na tayari uongozi ulimpa onyo la kuacha kuchochea mgomo kwa wasanii wengine ambao ni Charls Gabriel ‘Chalz Baba’ na Kalala Hamza Kalala ‘Kalala Junior’ kutoka African Stars ‘Twanga Pepeta’ na Jose Mara wa FM Academia.
“Huyu Chokoraa sasa amezidi kuwa mtovu wa nidhamu, pia aheshimu mkataba wake wa kazi, hivyo namsimisha hadi hapo tutakapomjadili na atalazimika ajieleze kwa uongozi kwa nini anafanya hivi,” alisema kwa hasira mwana mama huyo.
Alisema wiki iliyopita walimwonya naye akakiri kuacha tabia hiyo ambayo inaelekea kuweka rehani ajira yake Twanga.
Naye shabiki mmoja ambaye hakutaka kutajwa jina lake gazetini alisema kwamba wasanii hao wa Twanga watakuwa wakichuuzwa na Jose Mara wa FM Academia, hivyo wanatakiwa kuwa makini hata kama watakuwa na lengo la kuganga njaa.
Aidha, kundi hilo la wanamuziki wamepanga kujitambulisha rasmi kwenye ukumbi wa Sterio uliopo Kinondoni jijini Dar es Salaa, huku kila mmoja akipanga kuimba wimbo aliofyatua nje ya bendi.
|
|
|
Ismail Ally
|
|
|
|
|
|
|
|
Mtoa Maoni:
mama naso
Friday, November 27, 2009 15:06:49
|
|
Mtoa Maoni:
DeClarkes
Friday, November 27, 2009 18:16:34
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Habari zaidi za burudani |
...Habari Zaidi
|
|
Advertisements

|
|
Habari Zilizosomwa Sana |
|
|
|
|
| Photo Gallery |
 |
|
|
 |
|
|
|
|
|
|
|