|
|
|
Rihanna Akanusha Kumhonga Penzi Jay-Z |

Rihanna |
Tuesday, November 24, 2009 5:45 PM
Nyota wa muziki wa R&B wa Marekani Rihanna amekanusha uvumi uliozagaa nchini Barbados alikozaliwa kuwa alimhonga penzi mkongwe wa hip hop Jay-Z ili apate umaarufu alio nao sasa. |
Nyota wa muziki wa R&B wa Marekani aliyetamba na nyimbo yake ya "Umbrella" ameelezea kuchukizwa na uvumi uliozagaa wakati alipoanza kuwika kwenye anga ya muziki kuwa alimhonga penzi Jay-Z ili ampe tafu kwenye masuala ya kimuziki.
Kipaji cha muziki cha Rihanna kilivumbuliwa kwenye visiwa vya Barbados na Jay-Z ambaye aliamua kumpa tafu Rihanna kuandaa albamu yake ya kwanza.
Lakini Rihanna anasema kuwa uvumi ulizagaa kila kona kwenye visiwa hivyo kuwa alimpa uroda Jay-Z ili ampe tafu kimuziki.
Rihanna anasema kuwa hata marafiki zake wa karibu waliamini kuwa alilala na Jay-Z ili apewe tafu.
Rihanna amekanusha uvumi huo na kusema kuwa hakuwahi kuwa na uhusiano wowote wa kimapenzi na Jay-Z.
"Uvumi huu ulinifanya nijisikie vibaya wakati wote na nilishindwa hata kumuangalia machoni Jay-Z", alisema Rihanna.
"Siku moja Jay-Z aliniita na kuniambia nisisikilize watu wanachovumisha, nisiishi kwa kufuatisha maneno ya watu", alisema Rihanna. |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Mtoa Maoni:
Ubuguvu
Tuesday, November 24, 2009 18:29:54
|
|
Mtoa Maoni:
kipara
Tuesday, November 24, 2009 18:41:30
|
|
Mtoa Maoni:
amankwa
Tuesday, November 24, 2009 20:04:41
|
|
Mtoa Maoni:
moms016
Tuesday, November 24, 2009 23:43:02
|
|
Mtoa Maoni:
pumbundefu
Tuesday, November 24, 2009 23:50:05
|
|
|
|
|
|
Jumla kuna maoni (9), Soma maoni yote |
|
|
|
|
|
|
|
Habari zaidi za burudani |
...Habari Zaidi
|
|
Advertisements

|
|
Habari Zilizosomwa Sana |
|
|
|
|
| Photo Gallery |
 |
|
|
 |
|
|
|
|
|
|
|