|
|
|
Miss Tanzania Akabidhiwa Mkoko Wake |

MISS Tanzania 2009, Miriam Gerald akiwa na gari lake |
Wednesday, November 04, 2009 7:50 PM
MISS Tanzania 2009, Miriam Gerald amekabidhiwa rasmi gari lake aina ya Suzuki Grand Vitara lenye thamani ya Sh. milioni 53 ambalo limetolewa na wadhamini wa shindano hilo, Kampuni ya Huduma za Simu za Mkononi, Vodacom. |
Meneja Udhamini wa Vodacom, George Rwehumbiza amesema kuwa walichelewa kumkabidhi mrembo huyo zawadi yake kwa kuwa walikuwa bado hawajamaliza taratibu za usajili wa gari hilo.
Alisema kwa sasa ni wamemaliza kila kitu ikiwemo kubadilisha jina na kusajili jina la mrembo huyo na mambo mengine ambayo yatamfanya atambulike kuwa ndio mmiliki wa gari hilo.
Mwenyekiti wa Miss Tanzania, Hashim Lundenga aliwapongeza Vodacom kwa kutimiza ahadi yao ambayo walihaidi kabla ya kumpata mshindi huyo na kumtaka mrembo huyo kulitunza gari hilo kwani linathamani kubwa.
Pia, aliwataka wadhamini wasimuache peke yake mrembo huyo katika mambo mbali mbali ikiwemo hata ushauri kwa mrembo huyo pindi wanapomuona ameenda tofauti na utaratibu wa mashindano hayo.
Mrembo huyo anaondoka nchini wiki hii kwenda katika maandalizi ya mashindano ya dunia ambayo yatafanyika Johannesburg, Afrika Kusini Desemba 12.
Mrembo huyo anaagwa kesho katika ukumbi wa kituo cha uwekezaji TIC na mgeni rasmi katika hafla hiyo anakuwa Mkurugenzi wa TIC, Emmanuel Ole Naiko.
|
|
|
Ismail Ally
|
|
|
|
|
|
|
|
Mtoa Maoni:
moms016
Wednesday, November 04, 2009 22:30:23
|
|
Mtoa Maoni:
Ubuguvu
Thursday, November 05, 2009 00:26:28
|
|
Mtoa Maoni:
jmani
Saturday, November 21, 2009 18:35:35
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Habari zaidi za burudani |
...Habari Zaidi
|
|
Advertisements

|
|
Habari Zilizosomwa Sana |
|
|
|
|
| Photo Gallery |
 |
|
|
 |
|
|
|
|
|
|
|