|
|
|
Miss Tanzania Aanza Harakati Za Kutwaa Miss World |

MISS Tanzania 2009, Miriam Gerald |
Tuesday, October 20, 2009 4:56 PM
MISS Tanzania, Miriam Gerald, ameanza mazoezi ya kujindaa na shindano la kumsaka mrembo wa dunia linalotarajiwa kufanyika Desemba mwaka huu huko Afrika Kusini. |
Akizungumza na gazeti moja jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino inayoratibu shindano la Miss Tanzania, Hashimu Lundenga, alisema kwamba mrembo ameanza mazoezi hayo mapema ili aweze kufanya vizuri katika fainali za mwaka huu.
Lundenga alisema ili kuhakisha anakamilika kila idara, Miriam atakuwa akinolewa na walimu watatu ambao kila mmoja atakuwa na eneo lake.
“Moja ya mazoezi hayo ni kumjenga kisaikolojia, lugha ambayo itamuwezesha kukabiliana na waandishi wa habari wa mataifa mengine, waandaaji wa mashindano hayo na warembo wenzake.
Pia mrembo huyo atafundishwa masuala mbalimbali yanayohusiana na mashindano hayo ikiwemo jinsi ya kuvaa mavazi yanayoendana na muda sehemu na wakati.
Aliongeza kuwa tayari mrembo huyo amechukuliwa vipimo vyote muhimu na majibu yake kuwa safi ambapo kabla ya kwenda Afrika Kusini anatarajia kuhudhuria Mkutano wa Dunia wa Biashara utakaofanyika mapema Novemba nchini Uingereza.
|
|
|
Ismail Ally
|
|
|
|
|
|
|
|
Mtoa Maoni:
maua
Tuesday, October 20, 2009 19:31:51
|
|
Mtoa Maoni:
kipara
Tuesday, October 20, 2009 20:07:30
|
|
Mtoa Maoni:
moms016
Tuesday, October 20, 2009 21:49:37
|
|
Mtoa Maoni:
nyoshi
Wednesday, October 21, 2009 01:34:38
|
|
Mtoa Maoni:
Jembe
Wednesday, October 21, 2009 02:27:16
|
|
|
|
|
|
Jumla kuna maoni (12), Soma maoni yote |
|
|
|
|
|
|
|
Habari zaidi za burudani |
...Habari Zaidi
|
|
Advertisements

|
|
Habari Zilizosomwa Sana |
|
|
|
|
| Photo Gallery |
 |
|
|
 |
|
|
|
|
|
|
|