|
Aurora Yajitosa Miss Utalii Ilala 2009 |

Baadhi ya warembo wa Miss Utalii, 2009 |
Tuesday, October 20, 2009 4:53 PM
KAMPUNI ya Aurora Security imetoa sh mil. 25 kwa waandaaji wa shindano la kumsaka Miss Utalii Ilala 2009 ili kufanikisha shindano hilo. |
Fedha hizo zinajumuisha usafiri, chakula kwa warembo wakati wa kambi, pamoja na zawadi kwa mshindi wa kwanza hadi wa tatu.
Huu utakuwa muendelezo wa kampuni hiyo katika kusaidia kufanikisha mashindano ya Miss Utalii ambapo hivi karibuni ilidhamini shindano la Miss Utalii Temeke lililofanyika katika Ukumbi wa City Garden.
Kwa mujibu wa mratibu wa Miss Utalii Ilala, Amina Boke, shindano hilo linatarajiwa kufanyika Novemba 6 mwaka huu katika ukumbi wa Dar West Park uliopo Tabata, jijini Dar es Salaam.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Aurora Security, Ally Aurora, alisema kuwa wameamua kuendelea kusaidia Miss Utalii kutokana na kugundua ubora na umuhimu wa shindano hilo kwa Tanzania kwani linalenga kuitangaza Tanzania kupitia utalii na rasilimali zilizomo nchini ikiwa ni pamoja na vivutio vya utalii.
“Nitaendelea kuwapa msaada mtakaohitaji kwangu, ili muweze kufanya vizuri katika shindano lenu, kwani kupitia ninyi nchi yetu inaweza kutangazika ikiwa ni pamoja na kuvitangaza vivutio vyetu, pia ikiwa ni kuwapa changamoto,” alisema.
Aliongeza kuwa atakuwa akitoa mchango wake ili kuwezesha kuitangaza nchi iweze kujulikana kimataifa kwa kuendelea kuwapatia mahitaji mbalimbali washiriki wa mashindano hayo.
Warembo 12 wamejitokeza kushiriki shindano hilo ambao ni pamoja na Flora Nicholaus(22), Edna Andrew(20),Taus Thomas(21),Sheimaa Ntetema(20),Janneth Samson(19), Sheila Said Baamary(23),Sauda Ramadhani(22), Ratifa Iddy(20), Rechal Isaya(19), Jamida Abdu(21) na Tickey Lighton(21).
Mratibu huyo aliongeza kuwa milango bado iko wazi kwa warembo wengine watakaohitaji kushiriki shindano hilo kujitokeza katika Ukumbi wa Da West Inn Park, Tabata ilipo kambi ya warembo hao.
Mbali na Aurora, wadhamini wengine ni pamoja na Kelken Fitness Center, Dage Saloon, Kiwanga Store & C0, Aucland Tours & Safari, The Grand Villa Hotel, Mashujaa Pub, Sayona Drinks Water, Moringa Oleifera, Image Smart, Valley Spring na Mh. Mussa Azan Zungu. Wengine ni Papaa Msofe, VAM General Supply, Victor na Kariakoo, Mama Vanessa, makampuni ya simu za mkononi ya Tigo, Babu Kubwa na Magazine & OK News Week, Kiu, San, Mh. Idd Azan.
|
|
|
Ismail Ally
|
|
Mtoa Maoni:
rungu langu
Tuesday, October 20, 2009 19:48:51
|
|
Mtoa Maoni:
kipara
Tuesday, October 20, 2009 20:18:51
|
|
Mtoa Maoni:
moms016
Tuesday, October 20, 2009 21:56:54
|
|
Mtoa Maoni:
ubuguvu
Tuesday, October 20, 2009 22:40:44
|
|
|
|
|