|
|
|
Kichaa Avamia Shoo ya FM Academia na Kuvua Nguo |

Nwasuma si mchezo sema lilimuongezea ukichaa chizi huyu |
Tuesday, October 20, 2009 1:32 AM
Kichaa mmoja mwanaume usiku wa jumapili alivamia shoo ya bendi ya FM Academia wakati wakitumbuiza katika ukumbi wa New Msasani Club jijini Dar es Salaam na kutinga jukwaani kabla ya kuanza kunengua huku akivua nguo zake na kubakia na shuka. |
Kichaa mmoja usiku wa jumapili aliingia na kifurushi cha uchafu kwenye steji ambayo wapenzi wa FM Academia walijimwaga kulisakata ngwasuma na aliwaacha watu wengi wakipigwa na butwaa.
Walinzi wa ukumbi huo hawakujua chochote wakati watu waliupokuwa wakiukimbia ukumbi hasa sehemu ya steji maalumu kwaajili ya watu waliojitosa kulirudi Ngwasuma la FM Academia.
Kichaa huyo alionekana kuwa mjuzi zaidi wa kunengua baada ya kwenda sambamba na wanenguaji wa bendi hiyo na alitia fora zaidi wakati kiongozi wa bendi hiyo alipopanda kuimba wimbo wa Henken .
Muda jinsi ulivyokuwa ukienda ndivyo ukichaa wake ulipozidi kupanda hadi ilipofikia hatua ya kuvua nguo zake na kuvaa shuka ambalo alikuwa amelificha katika kifurushi chake cha taka taka ambazo zilizagaa eneo la kuchezea.
Hata hivyo waimbaji FM Academia walikerwa na kichaa huyo ambaye vituko vyake vilianza kuwaudhi watu wengi na kupelekea mpiga ngoma wa bendi hiyo kuziacha ngoma zake na kwenda kumtoa nje ya ukumbi kichaa huyo.
Mwandishi wa Nifahamishe alimfuata nje kichaa huyo na kumuuliza jina lake na bila kusita alijibu anaitwa "Dokta Andrew" na anaishi katika maeneo ya Mikocheni B.
Kuingia kwa kichaa huyo kwenye ukumbi mpaka kufika kwenye steji kuu kulionyesha kuwa ukumbi huo hauna ulinzi wa kutosha kutokana na kwamba kichaa huyo alipita kwenye geti lenye mabaunsa kibao ambao walikomaa usiku mzima kuhakikisha watu wenye tiketi pekee ndio wanaoingia ukumbini. |
|
  GONGA HAPA KWA PICHA ZAKE   |
Na Kaimanzila, Dar
|
|
|
|
|
|
|
|
Mtoa Maoni:
moms016
Tuesday, October 20, 2009 01:42:57
|
|
Mtoa Maoni:
edmundo
Tuesday, October 20, 2009 01:49:10
|
|
Mtoa Maoni:
Nautiakasi
Tuesday, October 20, 2009 02:37:21
|
|
Mtoa Maoni:
KING
Tuesday, October 20, 2009 10:06:55
|
|
Mtoa Maoni:
moms016
Tuesday, October 20, 2009 16:30:27
|
|
|
|
|
|
Jumla kuna maoni (6), Soma maoni yote |
|
|
|
|
|
|
|
Habari zaidi za burudani |
...Habari Zaidi
|
|
Advertisements

|
|
Habari Zilizosomwa Sana |
|
|
|
|
| Photo Gallery |
 |
|
|
 |
|
|
|
|
|
|
|