|
|
|
Wasanii wa Maigizo Nchini Watakiwa Kwenda Shule |

Steven Kanumba, miongoni mwa wasanii wa Bongo waliofanikiwa katika fani ya maigizo |
Monday, October 19, 2009 11:07 PM
WASANII wa sanaa ya uigizaji nchini, wametakiwa kujiendeleza kielimu ili kuweza kuendesha kazi yao kwa ufanisi zaidi na kuepuka hali iliyojitokeza siku hizi ambapo sanaa ya maigizo imekuwa kimbilio la watu walioshindwa maisha. |
Kauli hiyo imetolewa na mwalimu wa sanaa wa taasisi ya Youth Entertainment Campaign (YEC) Said Baraghash wakati taasisi hiyo ilipokuwa inazindua shindano la kusaka vipaji vya uigizaji la 'Ibua Filamu Star Tanzania' mapema wiki hii.
Baraghash alisema kuwa fani ya uigizaji kwa sasa imechukuliwa kama moja ya kimbilio la watu walioshindwa maisha, kitu ambacho ni hatari kwa maendeleo ya fani yenyewe.
Baraghash alisema kutokana na dhana hiyo washiriki walio wengi wamekuwa na mapungufu katika kutambua sheria na kanuni za fani hiyo hivyo kuwapa wakati mgumu kujenga uelewa wa wahusika.
Alisema katika mpango huo wa YEC, wanatarajia kuleta mapinduzi kwa kuwapa mafunzo ya saikolojia chipukizi watakaoshinda, kutokana na kile alichodai kuwa matatizo ya kisaikolojia ni tatizo kubwa kwa wasanii nchini.
"Kwa kweli tunakabiliwa na changamoto kubwa ya kuwajengea uelewa wasanii wa fani hii hasa wale watakaopatikana katika shindano hili la Ibua Filamu Star Tanzania," alisema Baraghash.
Kwa upande wake Meneja Mipango wa YEC Adam Seleman maarufu kama (Swebe) alisema shindano hili litachangia kuibua vipaji vya vijana ambao wanaonekana kuwa na fani ya uigizaji.
Swebe alisema kwa kuanza mashindano hayo yatashirikisha mikoa ya Arusha, Mwanza, Mbeya, Dodoma, Zanzibar na Dar es Salaam.
Meneja Mipango huyo alibainisha kuwa washiriki wanaohusika ni wenye umri kuanzia miaka 16 na kuendelea ambao hawajawahi kushiriki katika filamu yoyote.
Aidha alisema kupitia shindano hilo, wasanii watakaoonyesha viwango watashiriki katika filamu zitakazotolewa na kampuni hiyo ambazo zitasimama kuelezea mila na tamaduni za mtanzania.
Swebe alisema fomu za ushiriki zitatolewa katika mikoa husika ambapo siku ya mwisho ya kurudisha fomu hizo itakuwa Oktoba 30 mwaka huu na usahili utaanza Oktoba 31 Mjini Arusha. |
|
|
Na Kaimanzila, Dar
|
|
|
|
|
|
|
|
Mtoa Maoni:
moms016
Tuesday, October 20, 2009 01:48:59
|
|
Mtoa Maoni:
KING
Tuesday, October 20, 2009 10:15:25
|
|
Mtoa Maoni:
josephina msuya
Sunday, November 01, 2009 14:09:31
|
|
Mtoa Maoni:
jenny backpacke
Sunday, November 01, 2009 14:15:52
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Habari zaidi za burudani |
...Habari Zaidi
|
|
Advertisements

|
|
Habari Zilizosomwa Sana |
|
|
|
|
| Photo Gallery |
 |
|
|
 |
|
|
|
|
|
|
|