|
|
|
Yanga Kuwashughulikia Watovu Wa Nidhamu |

Amir Maftah |
Friday, February 05, 2010 11:20 AM
UONGOZI wa Yanga umesema utawajadili wachezaji wake wanaonyesha utovu wa nidhamu Uwanjani. |
Katika mechi mbili mfululizo, Yanga imekuwa ikimaliza mechi zake wakiwa pungufu kutokana na wachezaji wake kutolewa kwa kadi nyekundu.
Katika mchezo dhidi ya Majimaji, beki wa kutumainiwa wa timu hiyo, Wisdom Ndlovu alitolewa kwa kadi nyekundu na katika mechi yake dhidi ya JKT Ruvu, Amir Maftah naye alitolewa kwa kadi hiyo hiyo.
Afisa Habari za timu hiyo, Louis Sendeu aliliambia gazeti moja la kila siku kwamba, uongozi umestushwa na tabia hiyo ambayo inatakiwa kurekebishwa mara moja.
Sendeu alisema kuwa Yanga inakabiliwa na mashindano makubwa ya Ligi ya Mabingwa Afrika na wachezaji wake wanatakiwa kuwa makini sana na kadi zisizo kuwa na msingi.
"li ni tatizo kwa wachezaji wetu, hata hivyo tutakaa na wachezaji hao na kuongea nao ili kutatua tatizo hilo" alisema Sendeu.
Katika mechi ya juzi, Maftah alipewa kadi mbili za njano kwa kujitakia mwenyewe.
Mwamuzi, Klina Kabala wa Dar es Salaam aliwaamuru wachezaji wa Yanga waende kwenye ukuta ili adhabu hiyo ipigwe, Maftah akatoka na kwenda kuchelewesha mpira.
Katika kadi ya pili, Maftah alimpiga ngumi mchezaji wa JKT Ruvu wakati huo mchezaji mwezake, Bakari Mbegu akiwa amekwisha okoa mpira.
Mwamuzi wa pembeni, Godfrey Tumaini alimuona na kumwita mwamuzi wa kati na kumpa kadi nyekundu.
|
|
|
Ismail Ally
|
|
|
|
|
|
|
|
Mtoa Maoni:
Ubuguvu
Friday, February 05, 2010 13:28:52
|
|
Mtoa Maoni:
KING
Friday, February 05, 2010 16:21:13
|
|
Mtoa Maoni:
Semenya
Friday, February 05, 2010 21:41:08
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
Habari zaidi za michezo |
...Habari Zaidi
|
|
Advertisements

|
|
Habari Zilizosomwa Sana |
|
|
|
|
| Photo Gallery |
 |
|
|
 |
|
|
|
|
|
|
|