Tangaza Hapa Email: sales@nifahamishe.com
   
 
Member's Login
Username
Password
Not a member? Sign Up
            Sign Out

 
 
Mama Mdogo Kuliko Wote duniani Kujifungua Mtoto wa Tatu


Stacey Herald anatarajia mtoto wa tatu ingawa madaktari wamemuonya maisha yake yako hatarini
Friday, November 13, 2009 6:46 AM
Mama mwenye umbile dogo kuliko wote duniani anatarajia kujifungua mtoto wa tatu ingawa madaktari wamemuonya kuwa maisha yake yako hatarini kutokana na tumbo lake kuwa kubwa sana kuliko mwili wake kiasi cha kumfanya ashindwe hata kutembea.
Stacey Herald, ambaye ana urefu wa sentimeta 71 anatarajia kujifungua mtoto wa tatu ingawa madaktari wameendelea kumuonya kuwa maisha yake yako hatarini kutokana na mimba aliyonayo.

Stacey alishayapuuza maoni ya madaktari mara mbili na kufanikiwa kujifungua watoto wawili ambao urefu wao wakati walipozaliwa ulikuwa ni zaidi ya nusu ya urefu wake.

Stacey mwenye umri wa miaka 35 mkazi wa Dry Ridge, Kentucky nchini Marekani anasumbuliwa na ugonjwa unaoitwa Osteogenesis Imperfecta, ambao husababisha mifupa kuwa dhaifu yenye kuvunjika kirahisi, mapafu dhoofu na ugonjwa huo umemsababishia asirefuke.

Stacey anaishi na mumewe Will mwenye urefu wa mita 1.75 na wanatarajia kupata mtoto wa tatu ndani ya wiki nne zijazo.

Kutokana na ukubwa wa tumbo lake la ujauzito, Stacey hawezi kufanya kazi yoyote ya nyumbani na humtegemea mumewe kufanya kazi hizo.

Kwa jinsi alivyo mfupi, mtoto wake atakayemzaa atakapofikisha umri wa mwaka mmoja atakuwa tayari ameishamzidi kwa urefu.

Pamoja na vikwazo vyote, wanandoa hao ambao walivalishana pingu za maisha mwaka 2004, wamesema wangependa kupata watoto zaidi.

Lakini madaktari wamemuonya Stacey kuwa mtoto aliye tumboni mwake anaendelea kukua na umbile lake litakuwa kubwa zaidi kuliko mwili wake mdogo na hivyo kupelekea viungo vyake vya ndani kupasuka na kupelekea kifo chake.

Hata hivyo Stacey amepania kuendelea na ujauzito wake kama mimba zake mbili zilizopita ambazo aliambiwa maneno kama hayo lakini aliyapuuza na kuzaa salama.

Mtoto wake wa kwanza Kateri alizaliwa mwaka 2006 akiwa na urefu nusu ya urefu wa mama yake kwa bahati mbaya alirithi ugonjwa wa mama yake kwahiyo naye pia hatarefuka atakuwa kama mama yake.

Stacey alipata mimba kwa mara nyingine mwaka uliofutia na alijifungua mtoto mwingine wa kike aliyepewa jina la Makaya.

Hivi sasa watoto wake wote wawili wana urefu zaidi ya mama yao.
  GONGA HAPA KWA PICHA ZA STACEY NA FAMILIA YAKE  

 
Source: News Agencies    
Mtumie Rafiki Yako
  Comments    Add your Comment

Mtoa Maoni: Ubuguvu    Friday, November 13, 2009 10:17:50   
 
Kwanza na mpongeza kwa kupata watoto na kua na moyo wakuta kuendea na kupata watoto zaidi na hasa kutokana na hali yake hapo baadae watamsaidia sana wakikua ni mamuzi ya kungwa mkuno na hasa ukingati huku majuu wanawake wengi wanatoa mimba na huko tz wanatupa watoto chooni lakini ushauri wa daktari ni muhimu kufaatwa kama mimc hii akijifungua salama bora ajizuie kupata mimba na nampongeza pia kwa mwanaume alitumia umahiri mkubwa mpaka akamfika ktk nanii au walipandika mbegu
 
 
Mtoa Maoni: ShaMusua    Friday, November 13, 2009 15:11:59   
 
Jamani, tuseme kweli wanaume hivi hata huruma hatuna??? inakuaje kumtendea mama kama huyu?? wanambaka au analilia????
 
 
Mtoa Maoni: moms016    Friday, November 13, 2009 15:40:35   
 
"Je munaonaje manii muyatumbukizayo katika tumbo la uzazi? hivyo ninyi ndio munaoumba au sisi?" maneno ya kweli.. Ushauri wa daktari huwa kweli na haupingiki, lkn pamoja na yote kuna kudura isiyoingiliwa na kiumbe yyt. Kajifungua 2 za mwanzo na tunamuombea na ya 3 kwa kwenda mbele zitinge hewani.. inshalah. kwani c "ke" na anahitaji wtt?
UBUGUVU usishangae mkono hautafuti kinywa hata gizani unajua mdomo uko wapi!

 
 
Mtoa Maoni: mark.mushi    Friday, November 13, 2009 21:22:18   
 
duh e bwana hee ubuguvu umeongea point kweli,duh ata mimi nafikiri alimuweka juu ya meza adi kufikia down,sasa anazaa kwa operesheni au?
 
 
Mtoa Maoni: ShaMusua     Saturday, November 14, 2009 09:37:25   
 
hata kama ni njaa moms016 hekima itumike!!! kupitisha majamaa hali unajua hali ya mwenzako!!! mwenye mzigo hakutumia busara japo kwa dk 4

 
 
      
Unakaribishwa kuchangia maoni yako
Jina Lako    *
Maoni Yako *
 
*** Unaruhusiwa kutuma maoni yako yoyote yale. Tafadhali tumia lugha nzuri, maoni yenye kukashifu watu na yasiyofaa kwa jamii hayataruhusiwa. ***

*** Maoni yanayotolewa hapa ni mawazo binafsi ya Mtoa Maoni
Nifahamishe.com Haihusiki na maoni yatakayotolewa ***
More life style news and articles
> Urefu Wasababisha Aache Shule ya Msingi
> VIDEO - Nywele Zilizokatiwa Bima ya Dola Milioni 1
> Kweli Mapenzi Hayana Umri...
> Mtoto Mnene Kuliko Wote Duniani
> Maisha Yake Yapo Hatarini Iwapo Atalala
> Utamu na Faida za Tende
> Madada Wanne Wazaa Watoto Wanne Ndani ya Siku Nne
> Babu Aota Mmea wa Njegere Kwenye Mapafu
> Akataa Tsh. Milioni 500 Ili Asiolewe
> Auza Bikira Yake Kwa Tsh. Milioni 500
> 'Mwanaume Mjamzito' Kujifungua Mtoto wa Tatu
> Operesheni za Kurudisha Bikira Zawa Dili Uingereza
> Matiti Yapigwa Pasi Ili Kuzuia Watoto Wasibakwe
> Inakuwaje Wanigeria Wakazaa Mtoto Mzungu?
> VIDEO - Apewa Mkong'oto na Kuozeshwa Mke Kinguvu
> Mrembo Mwenye Matiti Makubwa Kuliko Wote Duniani Apigania Maisha Yake
> Mjadala wa Yai na Kuku Kipi Kilianza Wapata Jibu la Kisayansi
> Nyota wa Filamu za Ngono Anapokuwa Mwalimu wa Sekondari..
> Keki ya Bethidei Kutimiza Miaka 130
> VIDEO - Mtoto Azaliwa na Sura Yenye Kinyago China
> Ili Asifariki Analazimika Kula Kila Baada ya Dakika 15
> Afariki Baada ya Kupewa Taarifa ya Kifo Chake
> Watu Wafupi Wako Kwenye Hatari ya Kufa Kwa Magonjwa ya Moyo
> Hatimaye Sio Mungu Tena..
> Baada ya Ajali Mtoto wa Miaka 3 Awa Chapombe na Mvutaji Sigara

...Habari Zaidi

 

Advertisements
Tangaza Hapa Email: sales@nifahamishe.com
Habari Zilizosomwa Sana
1 Siri ya Kimada Yafichuka
2 VIDEO - Mwanaume Anayemchezea...
3 Ajinyonga Baada ya Kunyimwa M...
4 Kampeni zachachamaa, wapinzan...
5 JK aendelea kutoa ahadi
6 Pingamizi la Chadema baada ya...
Photo Gallery
Photo Album

 Ukisikia Wazazi bomu
Random Photo

 Jifotoe mama
Habari Mpya Mpya
> Siri ya Kimada Yafichuka
> Ajinyonga Baada ya Kunyimwa Mkopo
> VIDEO - Mwanaume Anayemchezea Simba Sharubu
> Kampeni zachachamaa, wapinzani nao watoa ahadi
> JK aendelea kutoa ahadi
> Pingamizi la Chadema baada ya siku 5
> Urefu Wasababisha Aache Shule ya Msingi
> Miaka 9 Jela Kwa Kuendesha Gari Huku Akiangalia Ngono
> VIDEO - Nywele Zilizokatiwa Bima ya Dola Milioni 1
> Kama Siku ya Kufa Haijafika...